MADIBIRA TUNA KAA WATU
Ni jambo la kusikitisha kuona wananchi wa Madibira wakitazamwa kama wanyama wasio na uelewa wowote juu ya dunia hii.Watu mbalimbali wenye nafasi serikalini na wanasiasa wana ifanya sehemu hii kama sehemu isiyo na wanadamu au kama wapo hawana uelewa wowote.
KILIMO
Mwaka 1997 mradi wa kilimo cha umwagiliaji ulianzishwa Madibira na serikali ukiwa na eneo la hekta 6000 sawa na ekari 15000 ambazo zilizungushiwa tuta, shamba hili kubwa la umwagiliaji lipo chini ya wananchi wa kawaida. Shamba hili ni sawa na eneo lililoachwa linalo limwa na wananchi ambao wapo nje ya huo mradi.
Madibira nai moja ya wazalishaji wakubwa wa mpunga kwa Afrika Mashariki na kati, licha ya jitihada hizo serikali bado ipo mbali na watu hao.
KIAFYA
Toka miaka ya 70 ilijengwa zahanati ambayo baadae ikawa kituo cha Afya mpaka sasa, idadi ya watu kipindi kituo hiki kinajengwa haikuwa kama ilivyo sasa. inakadiliwa kuwa kulikuwa na watu 8000 tu kipindi kituo hicho kikijengwa, kwasasa kuna watu zaidi ya 32000 sawa na ongezeko la asilimia 300. mwanzoni mwa miaka ya 2000 ulifanyika ukarabati wa majengo mawili yaliyo kuwepo na liliongezwa jengo moja lenye vyumba viwili tu ambalo kwasasa linatumika kama wodi ya wanaume na wanawake.Kwamuda sasa wanasiasa (wabunge na madiwani) kila atakaye kuwa anatafuta nafasi ya kisiasa lazima atagusia kuboresha mazingira ya hospitali hii na wakishinda wanapotea. Kutokana na ongezeko hili la wana wakazi kumekuwa na shida sana,serikali imekuwa ikileta dawa kutokana na rekodi za nyuma ,hii inapelekea dawa kuisha mapema toka siku ya kuletwa kwake. Majengo machache na vitanda kwaajili ya kulazwa wagonjwa ni vichache, alipo kuja mheshimiwa rais aliahidi kutatua kero zote za wana mbarali na madibira kwa ujumla lakini chenga tupu.ELIMU
No comments:
Post a Comment